Tuesday, June 13, 2017
Friday, March 31, 2017
MTIHANI WA DARASA LA SABA,19 NOVEMBA, 2015, SOMO URAIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA
MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) YA AWALI YA MKOA
DARASA LA SABA, 19
NOVEMBA, 2015
1. Soma
maelekezo yote yaliyotolewa kwa umakini.
2. Andika
jina lako, Wilaya, Shule na somo kwa
usahihi katika karatasi yako ya kujibia.
3. Jibu
maswali yote katika kila sehemu.
4. Andika
herufi ya jibu sahihi kwa kila swali katika karatasi yako ya kujibia uliyopewa.
5. Simu
za mkononi haziruhusiwi ndani ya
chumba cha mtihani
Chagua
jibu lililosahihi na uandike herufi inayohusika mbele ya namba ya kila swali
katika karatasi yako ya kujibia uliyopewa
1. Katiba
yaTanzania inayofanyiwa Marekebisho sasa ni ya mwaka
a) 1961
b) 1965
c) 1964
d) 1977
e) 1967
2. Serikali
ya kijiji au mtaa imeundwa chini ya sheria ya __
a) Serikali
kuu
b) Bunge
c) Baraza
la mawaziri
d) Mahakama
kuu
e) Serikali za
mitaa
3. Waziri
mkuu akishateuliwa na Rais lazima athibitishwe na
_____________
a) Mahakama
b) Usalama
wa Taifa
c) Baraza
la mawaziri
d) Bunge
e) Spika
wa bunge
4. Katika
nchi mhimili wenye mamlaka
ya kuongoza na kuendesha nchi ni ..............
a) Jeshi
la Polisi
b) Bunge
c) Serikali
d) Mahakama
e e) Magereza
5. Mwenyekiti wa
Kamati ya ulinzi na usalama
wa Mkoa ni
a) Mkuu
wa Wilaya
b) Katibu tawala
wa Mkoa
c) Afisa utumishi
wa Mkoa
d) Mkuu wa Mkoa
e) Kamanda wa Polisi
wa Mkoa
6. Chombo
chenye wajibu wa kulinda amani na usalama wa Taifa ni _________
a) Kila
raia
b) Jeshi la
wananchi
c) Polisi
d) Usalama
wa Taifa
e) Mahakama
7. Umuhimu
wa utamaduni katika jamii zetu za kitanzania
ni ___
a) Kuitambulisha
jamii
b) Kuleta
michezo ya asili
c) Kuzuia
maendeleo
d) Kugawa
wananchi kwa kutumia ukabila
e) Kuburudisha
jamii
8. Kati
ya zifuatazo ipi ni mila potofu katika jamii zetu ____
a) Kupatiwa
elimu
b) Kulindwa
c) Ukeketaji
d) Ngoma
e) Maziko
9. Chombo
chenye wajibu wa kusimamia masuala ya fedha nchini Tanzania ni____________
a) VICOBA
b) Benki
ya wananchi (NMB)
c) Wizara
ya fedha
d) SACCOS
e) Benki kuu ya
Tanzania (BOT)
10. Uchumi
wa taifa la Tanzania hutegemea
zaidi ________
a) Biashara
b) Misitu
c) Kilimo
d) Viwanda
e) Madini.
11. Uchaguzi
mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu utakuwa ni uchaguzi wa ngapi tangu kuanzishwa mfumo wa vyama vingi nchini
Tanzania ___
a) 3
b) 4
c) 6
d) 5
e) 6
12. Tanzania
inaongozwa kwa mfumo wa aina ya _
a) Kiimla
b) Kimapinduzi
c) Kidemokrasia
d) Kibepari
e) Kikabaila
13. Shirika
la umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi ni ____
a) UNHCR
b) WHO
c) UNICEF
d) UNIDO
e) HABITAT
14. Ni
nchi ipi kati ya zifuatazo si mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
a) Tanzania
b) Kenya
c) Zambia
d) Uganda
e) Rwanda
15. Katibu
Mkuu wa sasa wa Umoja wa Mataifa anaitwa
a) Barrack
Obama
b) Asha
Rose Migiro
c) Koffi
Anan
d) Ban Ki –Moon
e) Hillary
Clinton
16. Waziri
Mkuu wa
kwanza wa Tanzania alikuwa
a) Mwl J.K Nyerere
b) Edward Moringe
Sokoine
c) Rashidi Mfaume
Kawawa
d) Salim
Ahmed Salim
e) Joseph Sinde
Warioba
17. Kiongozi
ambaye huteuliwa na Rais na kuapishwa na
mkuu wa mkoa ni ___
a) Mkuu wa wilaya
b) Katibu
Tawala wa Wilaya
c) Kamanda
wa Polisi wa Wilaya
d) Mkurugenzi
wa Wilaya
e) Wabunge
18. Chombo
chenye wajibu wa kusimamia haki za wananchi ni____________
a) Bunge
b) Katiba
c) Mahakama
d) Serikali
za mitaa
e) Vyama
vya siasa
Thursday, March 30, 2017
MTIHANI WA DARASA LA SABA, 2016 SOMO HISTORIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA
MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) YA AWALI YA MKOA
DARASA LA SABA, 2016
SOMO HISTORIA
MUDA: SAA 1:30 (4:30 – 6: 00 MCHANA)
19 NOVEMBA, 2015
1. Soma maelekezo yote yaliyotolewa kwa umakini.
2. Andika jina lako, Wilaya, Shule na somo kwa usahihi katika karatasi yako ya
kujibia.
3. Jibu maswali yote katika kila sehemu.
4. Andika herufi ya jibu sahihi kwa kila swali katika karatasi yako ya kujibia uliyopewa.
5. Simu za mkononi haziruhusiwi ndani ya chumba cha mtihani
1. Gavana wa mwisho wa kiingereza hapa Tanganyika alikuwa ____________
a) Sir. Donald Cameron
b) Sir Horacce Byatt
c) Carl Peters
d) Julius von Sodden
e) Sir Richard Turnbull
2. Sultani wa kwanza kuitawala Zanzibar aliitwa.....
a) Seyyid Said
b) Said Bargharash
c) Sultani Bin Jamshidi
d) Saidi Majid
e) Said Salum
3. Uchumi wa Kikoloni katika Tanganyika na Zanzibar ulihakikisha upatikanaji endelevu wa
a) Mahitaji
b) Malighafi
c) Watumwa
d) Elimu
e) Huduma
4. Azimio la Arusha lilitangazwa huko Arusha mwaka..............
a) 1961
b) 1962
c) 1964
d) 1967
e) 1977
5. Msingi mkuu wa uchumi wakati wa mfumo wa Ukabaila ni ____
a) Fedha
b) Ardhi
c) Binadamu
d) Utumwa
e) Mtaji
6. Lengo kuu la wakoloni kutawala Tanganyika na Zanzibar ilikuwa ni............
a) Kujenga viwanda vikubwa kama vya ulaya
b) Kuzalisha malighafi kwa gharama ndogo
c) Kuendeleza jamii za Tanganyika na Zanzibar
d) Kuleta malighafi bora kutoka Ulaya
e) Kuanzisha mashamba makubwa
7. Vyama vya TANU na ASP viliungana rasmi mnamo ……….
a) Tarehe 5 february, 1977
b) Tarehe 8 february, 1977
c) Tarehe 12 january, 1964
d) Tarehe 26 Aprili 1964
e) Tarehe 5 July,1977
8. Gavana aliyeanzisha Baraza la kutunga sheria nchini Tanganyika aliitwa ...........
a) Richard Turnbul
b) Donald Cameroon
c) Edward Twinning
d) Horrace Byatt
e) John Scolt
9. Chifu Mangungo wa Msovero alisaini mkataba wa ulaghai na wakala wa Kiingereza aliyeitwa ----
a) Horace Byatty
b) Karl Peters
c) Julius Von Sodden
d) Willium Macknon e) Zelewisky
10. Mlinzi wa mali na familia katika jamii ya kimasai aliitwa____
a) Mtwa
b) Laiboni
c) Morani
d) Layoni
e) Mtemi
11. Mfumo wa Uongozi unaofuata misingi ya haki na sheria ni _____
a) Utawala wa kiimla
b) Utawala wa kisheria
c) Utawala bora
d) Utawala wa kidemokrasia
e) Utawala juu ya sheria
12. Taifa lililokomesha biashara ya utumwa katika Afrika Mashariki ni -------
a) Wajerumani
b) Wafaransa
c) Wareno
d) Waingereza
e) Waarabu
13. Mkutano wa kuligawa Bara la Afrika ulifanyika kati ya Mwaka
a) 1884 na 1885
b) 1886 na 1890
c) 1886 na 1888
d) 1845 na 1813
e) 1984 na 1985
14. Ngome ya Yesu (Forty Jesus) iliyojengwa na Wareno ilikuwa katika mji wa ___
a) Kilwa
b) Mombasa
c) Kalenga
d) Nairobi
e) Malindi
15. Wajerumani walijenga reli ya kati maeneo ya Pwani na Bara mnamo mwaka
a) 1897
b) 1900
c) 1905
d) 1960
e) 1805
16. Ni nchi ipi kati ya hizi haikutawaliwa na wakoloni?........
a) Angola
b) Tanzania
c) Ghana
d) Ethiopia
e) Zimbwabwe
17. Wakoloni wa kwanza kuitawala Tanganyika walikuwa __
a) Wereno
b) Wabeligiji
c) Waingereza
d)